Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, May 6, 2016

WATENDAJI WA VIJIJI WATAKIWA KUTO WACHANGISHA MICHANGO WALEMAVU YA UTEKELEZAJI MIRADI YA VIJIJI

 MWENYEKITI WA WALEMAVU WA MACHO LUSIUS MLOWEZI AKIENDESHA MKUTANO WA WALEMAVU  MKOA WA NJOMBE KWAMBA WAACHE OMBAOMBA INAWADHARIRISHA  WALEMAVU WENGINE



 AFISA USTAWI WA JAMII WA HALMSHAURI YA MJI WA NJOMBE HOSEA  YUSTO AKIZUNGUMZA NA WALEMAVU HAO NA KUAHIDI KUWATAFUTIA FIMBO NYEUPE  KWA WADAU WENYE  MAPENZI MEMA NA WALEMAVU HAO

 WALEMAVU WA MACHO WAKIWA NA MWENYEKITI WA CHAMA CHA WALEMAVU MKOA WA NJOMBE JACKSON FIHANGA AMBAYE NI MLEMAVU WA MIGUU ALIYEVAA BARAGASHIA NYEUPE AKISAIDIA KUANDIKA MIHTASARI
 HII NI TIMU YA WALEMAVU WA MACHO MKOA WA NJOMBE  WENGINE WAMETOKEA LUDEWA, WANGING'OMBE NA MAKAMBAKO


 AKIZUNGUMZA KWA NIABA YA AFISA USTAWI WA JAMII WILAYA YA NJOMBE AVERINO CHAULA  IGNASIA  MFAUME  AMETAKA WANANCHI KUTOWAFICHA WATU WENYE ULEMAVU KWANI NAO WANAHAKI KAMA WATU WASIYO NA ULEMAVU







Serikali Za Vijiji Na Kata Zimetakiwa Kuwatambua Watu Wenye Ulemavu Wa Viungo Mbalimbali Kwa Kuwapunguzia Tozo Za Michango Ya Utekelezaji Wa Miradi Iliyopo Kwenye Maeneo  Yao Hususani Watendaji Wa Vijiji Ambao Wamekuwa Wakiwalazimisha Walemavu Kuchangia Michango Licha Ya Kutambua   Ulemavu  Wa  Viungo Hivyo.

Wakizungumza Baadhi Ya Walemavu Wa Macho Wakiwa Kwenye Mkutano Wao  Wamesema  Wamekuwa Wakikabiliana Na Changamoto Mbalimbali Zikiwemo Za Kutozwa Michango Ya Utekelezaji Wa Miradi Kwa Lazima Hata Kama Hawana Uwezo Wa Kupata Fedha Hizo   Na  Kukosa Uwezo Wa Kufanya Kazi Ambazo Zinahatarisha Usalama Wao Kulingana Na Maumbile Walio Nayo.

Aidha  Walemavu Hao Pia Wameomba  Kupatiwa Vibali Vya  Matibabu Bure Kwenye Zahanati Na Hospitali Kwani Wanashindwa Kupata Fedha Ya Kuchangia Mfuko Wa Taifa Wa Bima Ya Afya  Na Kusababisha Wengine Kukosa   Huduma Za Matibabu Kutokana  Kukosa Fedha  Za Matibabu Huku  Walimu Wa Shule Za Msingi Na Sekondari Wakidaiwa Kuwanyanyasa Kwa  Kufukuza  Watoto Wao .

Lusius Mlowezi Ni Mwenyekiti Wa Walemavu Wa Macho Wilaya Ya Njombe  Ambaye Pamoja Na Kutaka Serikali Iwashirikishe Walemavu  Kwenye Vikao Vya  Maamuzi   Huku  Walemavu  Wakitakiwa Kuanzisha Vikundi  Vya Kiujasiliamali Ikiwemo Ufugaji Wa Kuku Kwa Manufaa Yao  Na Kuacha Kuomba Misaada Hovyo  Mitaani.

 Kwa Upande Wao Maafisa Ustawi Wa Jamii Wa Halmashauri Ya Mji Na Wilaya Ya Njombe  Hosea Yusto  Na Ignasia  Mfaume Wamepongeza Walemavu Wa Njombe  Kwa Kukemea Tabia Ya Kuomba Hovyo Misaada Kama Mikoa Mingine   Na Kutaka Waungane Pamoja Ili Wawe Na Sauti Ya Pamoja  Na Kuacha Kuwaficha Walemavu Nyumbani  Badala Yake Wawashawishi Wajiunge Kwenye Chama Hicho.


No comments:

Post a Comment