Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, May 1, 2016

SERIKALI MKOANI WA NJOMBE YAPATA HASARA YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 300 KWAAJILI YA WATUMISHI HEWA 108

 WAFANYAKAZI  WAKIWA KWENYE MAANDAMANO SIKU YA MEI MOSI MJINI MAKAMBAKO
 SKAUTI WAKIWA IMARA WAKATI MGENI RASMI AKITOA HOTUBA SIKU YA MEI MEI MOSI
 KIKUNDI CHA NGOMA KUTOKEA MWEMBETOGWA WAKITO   BURUDANI YA NGOMA YA ASILI

 MKUU WA MKOA WA NJOMBE DKT REHEMA NCHIMBI AKIWA JUKWAANI KUHUTUBIA SIKU YA MEIMOSI

HAPA ANAWAAPISHA WAFANYA KAZI WOTE KUWA WAADILIFU


Jumla Ya Watumishi Hewa  108 Wameisababishia Serikali Hasara Ya  Zaidi Ya Shilingi  Milioni Mia Tatu  Katika Halmashauri Za Mkoa Wa Njombe Ambapo Jitihada  Za Kuwabaini Watumishe Hewa Wengine Bado Zinaendelea  Na Kutaka Ushirikiano Ufanyike Baina Ya Vyama Vya Wafanya Kazi Na Serikali Kuwabaini Watumishi Hao Wasiyostahili.


Kauli Hiyo Imetolewa Na Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi   Kwenye Maadhimisho Ya Sikukuu Za Wafanyakazi Mei Mosi  Ambayo Kwa Mkoa Wa Njombe Yamefanyikia Katika Uwanja Wa Polisi Makambako  Na Kubainisha Watumishi Hewa Mia Moja Na Nane Ambao Wameisababishia Serikali Hasara Ya Jumla Ya Shilingi Milioni Mia Tatu  Tisini Na Mbili  Na Laki Nane.

Aidha Dkt Nchimbi  Amekiagiza Chama Cha Wafanya Kazi TUCTA Kwa Kushirikiana Na Vyama Vingine Vya Wafanyakazi Kuhakikisha Vinapeleka Majina Ya Watumishi Hewa  Ambao Wapo Kwenye Vyama Hivyo  Ndani Ya Mwezi Mmoja   Nakwamba  Wafanya Kazi Wamekuwa Wakilalamikia Serikali  Kuwatekelezea Mahitaji Yao Huku Baadhi Yao  Ni Watumishi Hewa Bila Kuwaondoa Kwenye Mfumo Wa Ajira Serikalini .

Katika Hatua Nyingine Dkt Nchimbi Amekitaka Chama Cha  Wafanyakazi TUCTA  Kuwatembelea Wahudumu  Wa Kwenye Biashara Za Bar  Kuhakikisha Wanapewa Mikataba  Na Waajili Wao  Agizo Ambazo Linatakiwa Kutekelezwa  Kwa Kipindi Cha Miezi Mitatu  Pamoja Na Kuwatembelea Wafanyakazi Wengine  Kubaini Matatizo Yanayowakabili.

Wakizungumza Na Uplands Fm Mara Baada Ya Hotuba Ya Mgeni Rasmi  Baadhi Ya Wafanyakazi Wa Mashambani  Wameipongeza Serikali Kwa Kuhimiza  Waajili Kuwalipa Ujira Unaotakiwa  Watumishi Wa Sekta Mbalimbali  Zikiwemo Sekta Binafsi   Huku Wakisema  Waajili Wengi Wamekuwa Wakiwakandamiza Wafanyakazi Wao Kwa Kuwalipa Ujira Mdogo.

Katika hatua nyingine Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe  Dkt Rehema Nchimbi Amezitaka Halmashauri  Za Mkoa Huo Kutenga Maeneo  Kwaajili Ya Viwanja Vya Kujenga Nyumba  Za Watumishi  Kwa Kuwatoza Fedha Kidogo  Kuliko Kuwapangishia Nyumba Zisizo Na Hadhi Na Kuchukua Kodi  Jambo Ambalo Limetajwa Kuwa Ni Kuwakandamiza Watumishi Hao.

 Dkt Nchimbi Ametaka Halmashauri Hizo Kutekeleza Agizo Hilo  Kwa Wakati Mara  Viongozi  Watakapo Kutana  Ili Watumishi Waweze Kujenga Nyumba Zao Na Kuimarisha Uchumi Kwa Kulima  Mashamba  Kwaajili Ya Matunda Aina Ya Parachichi.

Aidha Dkt Nchimbi Amesema Kuanzia Sasa Kila Mtumishi Mahala Anakoishi Anatakiwa  Kuwa Na Miti Ya Matunda Aidha Ya Parachichi  Kwaajili Ya Manufaa Ya Familia Zao Na Kukuza Uchumi Wa Kila Mmoja  Hatrua Ambayo Itahamasisha Wananchi Wengine Kuiga Mfano Huo Na Kuanzisha Kilimo Cha Matunda Huku Akiagiza Kila Shule  Kuwa Na Ekari Moja  Ya  Zao La Matunda Hususani Parachichi.

Dkt Nchimbi Amewaagiza Makatibu Tawala Wote Wa Wilaya Na Mkoa Kuhakikisha  Wanawachukulia Hatua Kali Za Kisheria Watumishi Wote Wanaokwenda  Kunywa Pombe Kwenye  Bar Na Virabu  Na Kusema Baadhi Ya  Biashara  Za Bar Zinatuhumiwa Kwa Kuhusika  Kuwauza Wasichana  Kingono  Jambo AMbalo Linatakiwa Kukemewa Na Kila Mmoja.

 Dkt Nchimbi Amezungumzia Uchumi Utakao Kuwepo  Mara Machimbo Ya Chuma Cha Liganga Na Makaa Ya Mawe  Kwenye Mgodi Wa Mchuchuma Wilayani Ludewa Ambapo Wananchi Wanatakiwa Kuwekeza Zaidi Kwenye Ufugaji,Kilimo Cha Matunda,Mbogamboga,Mahindi Na Mazao Mengine Kwaajili Ya Kuinua Uchumi Wao Ikiwemo Ufugaji.

Katika Kutekeleza  Kauli  Mbiu Ya Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe  Rehema Nchimbi Ya Kwamba Njombe Ni Lango Kuu La Uchumi, Baadhi  Ya Wakulima Wameanza Kutekeleza   Kauli Hiyo Akiwemo Daitan Mhema  Mkazi Wa Kijiji Cha Matiganjora Ambaye Ana Ekari  Takribani Tano Za Matunda Aina Ya Parachichi.
Maadhimisho hayo kwa siku ya leo yamebeba ujumbe usemao  DHANA YA MABADILIKO ILENGE KUINUA HALI ZA WAFANYA KAZI.

No comments:

Post a Comment