Wabunge
watatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Kangi Lugola
(Mbunge wa Mwibala), Mh. Sadiq Murad (Mbunge wa Mvomero) pamoja na Mh.
Victor Mwambalaswa (Mbunge wa jimbo la Lupa) wakiwa kwenye Mahakama ya
Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam, kwa kusikiliza kesi
inayowakabili ya kushawishi kupatiwa rushwa ya Mil. 30 kutoka kwa
mfanyabiashara mmoja hapa nchini.
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
WABUNGE watatu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za kuomba rushwa ya sh.milioni 30.
Wabunge waliofikishwa Mahakama ya Kisutu leo ni Mbunge wa Mvomero, Sadiq Murad, Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa, pamoja na Mbunge wa Mwibara Alphaxaid Kangi Lugola.
Mwendesha Mashitaka wa Tume ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mahela Ndimbo mbele Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba amesema tukio hilo lilitokea Machi 15 mwaka huu majira saa 2 had saa 4 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
Ndimbo alidai mahakamani hapo kuwa washitakiwa hao wakiwa wajumbe Kamati Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) waliomba rushwa ya sh.milioni 30 kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Gairo, Mbwana Magota.
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu,Thomas Simba alidai kuwa upande wa mashitaka upeleke ushaidi wa watuhumiwa wa rushwa .
Washitakiwa waliposomewa shitaka la kuomba rushwa wote walikana na dhamana yao kuwa wazi kwa masharti ya kila mmoja kwa na mdhamini wa mmoja wa sh.milioni tano pamoja na hati ya kusafiria ambapo wote walikidhi masharti ya dhamana hiyo.
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba ameairisha kesi hiyo mpaka Aprili 14 mwaka huu itakapotajwa tena .
WABUNGE watatu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za kuomba rushwa ya sh.milioni 30.
Wabunge waliofikishwa Mahakama ya Kisutu leo ni Mbunge wa Mvomero, Sadiq Murad, Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa, pamoja na Mbunge wa Mwibara Alphaxaid Kangi Lugola.
Mwendesha Mashitaka wa Tume ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mahela Ndimbo mbele Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba amesema tukio hilo lilitokea Machi 15 mwaka huu majira saa 2 had saa 4 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
Ndimbo alidai mahakamani hapo kuwa washitakiwa hao wakiwa wajumbe Kamati Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) waliomba rushwa ya sh.milioni 30 kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Gairo, Mbwana Magota.
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu,Thomas Simba alidai kuwa upande wa mashitaka upeleke ushaidi wa watuhumiwa wa rushwa .
Washitakiwa waliposomewa shitaka la kuomba rushwa wote walikana na dhamana yao kuwa wazi kwa masharti ya kila mmoja kwa na mdhamini wa mmoja wa sh.milioni tano pamoja na hati ya kusafiria ambapo wote walikidhi masharti ya dhamana hiyo.
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba ameairisha kesi hiyo mpaka Aprili 14 mwaka huu itakapotajwa tena .


No comments:
Post a Comment