Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, March 22, 2016

MWILI WA ALIYEKUWA MKUU WA WILAYA YA NJOMBE SARAH DUMBA UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA ILEMBULA KWAAJILI YA KUSAFIRISHWA KESHO MACH 23 KWAAJILI YA MAZISHI DAR ES SALAAM


Saraha DumbaAliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Bi. Sarah Dumba katika picha enzi za uhai wake.
....................................................................................
Mkuu wa Wilaya ya Njombe  Sara Dumba Amefariki  Baada ya Kuugua Ghafla Jana Jioni

Akitoa Taarifa za Kifo cha Mkuu wa Wilaya Hiyo , Mkuu wa Mkoa Dkt. Rehema Nchimbi Amesema Marehemu Amefariki Wakati Akiendelea na Matibabu Katika Hospitali ya Mkoa  wa Njombe (Kibena).

Kwa Mujibu wa Dkt.Nchimbi Amesema Kuwa Marehemu Sara Dumba Alifanya Kazi Zake

Kama Kawaidi Siku Nzima Hadi na Aliporejea Nyumba  na Kupata Chakula, na Kwamba Mara

Baada ya Kupata Chakula Hali Ilibadilika na Kuanza Kutapika Huku Akilalamika Kukosa Hewa

Ambapo Alipelekwa Hospitali Majira ya Saa 1:20 na Kufariki Wakati Akipatiwa Matibabu.

Dkt. Nchimbi Amesema Taratibu za Mazishi Bado Zinaendelea na Kwamba Kamati ya Ulinzi na

Usalama ya Mkoa wa Njombe Inakutana Leo Asubuhi Kupanga Ratiba Kamili.

Wakizungumza Na Waandishi Wa Habari Baadhi Ya Viongozi Wa Dini Waliofika Nyumbani

Kwa Marehemu Wamelezea Namna Walivyokuwa Wakishirikiana Na Aliyekuwa Mkuu Wa

Wilaya Ya Njombe Sarah Dumba  Wakati Wa Uhai Wake Kwamba Alihimiza Utekelezaji Wa

Miradi Ya Maji Na Kuwaunganisha Watumishi Wa Mungu Pasipo Kubagua Kanisa.
Kabla ya Kuteuliwa Mkuu wa Wilaya ya Njombe Marehemu Sara Dumba Alikuwa Mtangazaji wa Shirika la Habari Tanzania

Jamaa na  Familia ya Marehemu Sara Dumba Pamoja na Uongozi wa Wilaya ya Njombe Hasa Katika Kipindi Hiki cha Majonzi.

Mungu Alitoa na Mungu Ametwaa Jina la Bwana Lihimidiwe, Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Ma Hali Pema Peponi , Amen

No comments:

Post a Comment