Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, December 17, 2015

JESHI LA POLISI MKOA WA NJOMBE LA MSHIKILIA FROLA MSIGWA 39 KWA TUHUMA ZA WIZI WA MTOTO


 BIBI WA ALEN MAKWETA AKIWA KATIKA KAMBI AMBAKO MTOTO HUYO ALIIBIWA KARIBU NA HOSPITALI YA KIBENA
mwenyekiti wa serikali Ya Mtaa Wa Kibena Hospitali Winfred Kayombo  Kupitia CHADEMA


  KAMANDA WA JESHI LA POLISI MKOA WA NJOMBE WILBROAD MUTAFUNGWA AKITOA TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI



HAPA NDIPO MTOTO HUYO ALIIBIWA NA KUPATIKANA MAKAMBAKO KATA YA MJIMWEMA






Jeshi la Polisi Mkoani Njombe Linamshikilia Frola Msigwa Mwenye Umri wa Miaka 39 Mkazi wa

Mjimwema Makambako  Kwa Tuhuma za Kumuiba Mtoto Alen Makweta Mwenye Umri wa Miezi

Mitatu Katika Hospitali ya Mkoa wa Njombe Iliyoko Eneo la Kibena.

Kwa Mujibu wa Taarifa ya Jeshi la Polisi Iliyotolewa Kwa Vyombo Vya Habari na Kusainiwa na

Kamanda wa Jeshi Hilo Mkoa wa Njombe Wilbroad Mutafungwa Inasema Kuwa Tukio Hilo

Limetokea Decemba 16 Majira Saa Saba Mchana Katika Hospitali Hiyo,na Kwamba Mtuhumiwa

Amekamatwa Maeneo ya Makambako Akiwa na Mtoto Huyo.

Aidha Taarifa Hiyo Inaeleza Kuwa Jeshi la Polisi Linaendelea na Uchunguzi Dhidi ya Tukio Hilo na

Mara Uchunguzi Utakapokamilia Mtuhumiwa Atafikishwa Mahakamani Kujibu Tuhuma

Zinazomkabili, Huku Jeshi Hilo Likitoa Wito Kwa Kinamama Kuwa Makini Ikiwa ni Pamoja na

Kutowaachia Watoto Wao Watu Wasiowafahamu.

Upland's Redio Imezungumza na Mwenyekiti wa Mtaa wa Kibena Hospitali Winfred Kayombo

Ambaye Amethibitisha Kutokea Kwa Tukio Hilo Huku akiwasihi kina mama kuwa makini na malezi ya watoto wao ikiwemo kuwa nao karibu wakati wote .

Kwa Upande Wao Wazazi Wa Mtoto  Aliyeibiwa   Katika Eneo La Hospitali Ya  Kibena

Wameushukuru Uongozi wa Mtaa Huo , Wananchi Pamoja na Jeshi la Polisi Kwa Kufanikisha

Kupatikana Kwa Mtoto Wao Huku Wakielezea Mazingira Alivyoibiwa.


Nao Baadhi ya Wananchi Waliozungumza na Kituo Hiki Wameiomba Serikali ya Mkoa wa Njombe

Kuboresha Mazingira ya Hospitali Hiyo Ikiwemo Ulinzi na Kujenga Uzio Ambao Utasaidia kuzuia

Matukio Kama Hayo Katika Hospitali Hiyo Kupungua.


No comments:

Post a Comment