Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, September 21, 2015

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA NJOMBE KUSINI KUPITIA ACT WAZARENDO EMILIAN MSIGWA AENDELEA NA KAMPENI ZAKE UTENGULE

Mgombea Ubunge Jimbo La Njombe Kusini Kupitia Chama Cha ACT Wazalendo Emilian Msigwa Ameahidi Kuboresha  Uchumi Wa Halmashauri  Ya Mji Wa Njombe  Na Kutoa Ajira Kwa Vijana  Kupitia Mradi Wa Mabwawa Ya Samaki  Ambayo  Atakwenda Kuanzisha  Endapo Wananchi Watampatia Ridhaa Ya Kuongoza.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Mgombea Ubunge  Emilian Msigwa Wakati Wa Muendelezo Wa Kampeni Zake Akiwa  Kijiji Cha Utengule   Ambako Ameahidi  Kuondoa Umasikini  Kwa Wananchi Kwa Kutoa Mbinu  Mbadala Za Maendeleo  Ya Kila Mwananchi  Ikiwemo Kushawishi Kujiunga Kwenye Vikundi Na Kupata Mikopo Kwenye  Tasisi Za Kifedha.

Bwana Msigwa Amesema Kuwa   Endapo Wananchi Watampa Ridhaa Ya Kuongoza Jimbo La Njombe Kusini Hatua   Ya  Utekelezaji Wa Miradi Ya Halmashauri,Kata Na Vijiji  Atahakikisha  Unafuata Misingi Na Kanuni Za Kisheria Ikiwemo  Kuwapunguzia Michango Wananchi  Ambao Walibebeshwa Mzigo Mkubwa Na Halmashauri Ya Mji Wa Njombe.

Swala La Miundo Mbinu Ya Barabara Za Kuunganisha Vijiji Mbalimbali  Amesema Ataipa Kipaumbele  Ambapo Baadhi Ya Majukumu Alikwisha Anza Kutekeleza Kabla Ya Kugombea Nafasi Ya Ubunge Jimbo La Njombe Kusini Ikiwemo Kusomesha  Baadhi Ya Watoto Yatima  Pamoja Na Kuboresha Miundombinu Ya Barabara.

Kwa Upande Wake Wananchi   Wa Kijiji Cha Utengule Wameshukuru Kwa Kufika Na Kutoa Ahadi Hizo  Na Kusema Kuwa Emilian  Msigwa Wanamufahamu   Kama Mtoto Wa Nyumbani Kwao   Na Kuahidi Kumpatia Kura Za Kishindo Ifikapo Octoba 25 Mwaka Huu Huku Wakimpongeza Kwa Jitihada Za Kusomesha Watoto  Yatima Na Wasiyojiweza.

No comments:

Post a Comment