Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi
CCM Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi katika mkutano wake
wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa shule ya Msingi Kalangalala
mjini Geita leo na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi.
Mgombea
Urais Huyo amewaambia wananchi wa Geita kuwa mara atakapoingia Ikulu,
moja ya changamoto anazotarajiwa kuzipa kipaumbele ni pamoja na suala la
kutatua mgogoro wa wachimbaji madini wadogo wadogo.
Magufuli
ameasema kuwa akiingia madarakani atawapa maeneo wachimbaji wadogo wa
madini nchini ikiwa ni pamoja na kuwakopesha mitaji na kuwapa vifaa vya
kisasa vya kufanyia kazi zao pamoja na mafunzo kwa ajili ya kuboresha
uchimabaji wao ili uwe wa kisasa zaidi na kupandisha kiwango
cha ufanisi wa kazi zao za uchimbaji.
Dkt.
Magufuli leo amehutubia mikutano katika miji ya Runzewe wilayani
Bukombe, Katoro wilayani Chato na Geita mjini akiendelea na kampeni zake
za kwaomba wananchi kumpa kura za ndiyo ili aweze kuingia Ikulu na
kuwafanyia kazi Watanzania kama kiongozi na Amiri Jeshi mkuu wa
Tanzania.
Wananchi
wa mji wa Geita na vitongoji vyake wakiwa wamefurika kwenye uwanja wa
shule ya msingi ya Kalangalala,wakimsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania,kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe
Magufuli alipokuwa akijinadi na kumwaga sera zake mbele za wananchi hao
ikiwemo pia na kuwaomba ridhaa ya kuwa Rais kwa kushinda kura nyingi
ifikapo Oktoba 25 mwaka huu,ambapo uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika.
Mgombea
Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwandani Wagombea Ubunge wa
jimbo la Busanda Mh.Lolensia Bukwimba na Dkt Meedad wa Chato mapema
mchana huu alipokuwa akiwahutubia wananchi wa mji mdogo wa Katoro mkoani
Geita, kwenye viwanja vya mnada wa Ng'ombe,katika mkutano wa hadhara wa
kampeni,ambapo maelfu ya Wananchi wamehudhuria.Dkt Magufuli atahutubia
jioni ya leo mjini Geita kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
Mgombea
Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa mji mdogo
wa Katoro mkoani Geita mapema leo mchana kwenye viwanja vya mnada wa
Ng'ombe,kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni,ambapo maelfu ya Wananchi
wamehudhuria.
Wananchi wa Runzewe wakimsikiliza Dkt Magufuli alipokuwa akihutubia kwenye mkutano wa kampeni.
Mwenyekiti
wa CCM mkoa wa Geita na mgombea ubunge wa jimbo la Geita vijijini Ndugu
Joseph Kasheku a.k.a King Msukuma akihutubia malefu ya wananchi wa
Geita mjini kwenye mkutano wa kampeni wa Urais,ambapo Ndugu Joseph
aliwaomba wakazi wa Geita na vitongoji vyake kumchagua Dkt John Pombe
Magufuli awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu ya
tano,katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 25 mwaka.
Magufuli Style ilitikisa pia ndani ya Geita kwenye mkutano wa kampeni wa Dkt John Pombe Magufuli jioni ya leo.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi
CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwapokea mlemavu wa ngozi Albino Lazaro
Malendeka kushoto ambaye alikuwa mtumishi wa kikundi cha Red Briged cha
Chadema baada ya kujiunga na CCM mjini Geita leo na William Mabula
Msalaba aliyekuwa mgombea ubunge wa Chadema jimbo la Geita.

Wananchi wa Katoro wakiushangilia msafara wa Dkt Magufuli alipokuwa akielekea kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.







No comments:
Post a Comment