Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, August 6, 2015

TAMISEMI YAKABIDHI MADAWATI MUFINDI

Na Francis Godwin Iringa

Halmashauri za Wilaya ya Mufindi zimepokea jumla ya madawati ya kisasa 400 kutoka Wizara ya tawala za Mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI ikiwa niutekelezaji wa ahadi ya serikali ya kuzitumia fedha za chenji ya rada katika kuboresha elimu nchi.
Taarifa iliyotolewa na Ofisa habari na mawasiliano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Bw. Ndimmyake Mwakapiso ametanabaisha kuwa, madawati hayo yaliyotengenezwa kwa kuzingatia umri wa wanafunzi, yatasambazwa katika shule 10 za msingi wilayani humo. 
Aidha, Mwakapiso imevitaja vigezo ilivyotumika kutoa kipaumbele katika shule hizo kuwa ni pamoja na mgawavyo wa majimbo na halmashauri, uhaba wa madawati uliopo kwa kila shule sanjari na kigezo cha upya wa shule husika, ambapo halamashauri ya wilaya yenye shule 144 na majimbo 02 imepata madawati 320 kwa shule 8 huku Halmashauri ya mji wa Mafinga yenye shule 33 na jimbo moja ikipata madawati 80 kwa shule 02.
Shule zilizonufaika na madawati hayo kwa wilaya ya Mufindi ni shule za msingi Ikweha., Kipanga “A”, Ilasa, Igomaa na Mlimani nyingene ni Nzivi, Ihegela na Sawala, wakati halmashauri ya mji  Mafinga ni shule mpya ya msingi Mwongozo na shule ya msingi Kilimani.
.//////////////////////////////////MWISHO/////////////////////////

No comments:

Post a Comment