Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, June 26, 2015

MWENGE WA UHURU UMEPOKELEWA NJOMBE NA KUWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA SURPLISE BEACH MAKAMBAKO



















































































Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi Jana Amepokea Mwenge Wa

Uhuru Kutoka Kwa Mkuu Wa Mkoa Wa Iringa Amina MaSenze Ambao Baada

Ya Kupokelewa Katika Mtaa Wa Kipagamo Ulitembelea Na Kuzindua

Miradi Mbalimbali Ya Halmashauri Ya Mji Wa Makambako Ikiwemo Nyumba

Tano Za Watumishi Wa Makambako.

Akipokea Mwenge Huo Kwa Mkuu Wa Mkoa Wa Iringa Amina  Masenza, Mkuu

Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi  Amesema  Mwenge Huo Kwa Mkoa

Wa Njombe Utatembelea,Kuzindua Na Kuweka Mawe Ya Msingi Kwenye

Miradi 45 Yenye Thamani Ya Zaidi Ya Shilingi Bilioni 13 Na

Utakabidhiwa Julai Mosi Mkoani Mbeya Huku Mkoani Iringa Ukiwa

Umekimbizwa Kilomita 622 Na Kupitia Miradi 35 Yenye Thamani Ya

Shilingi Bilioni 4.

Miradi Mingine Iliyozinduliwa Na Kutembelewa  Na Mwenge Huo Ni

Pamoja Na Bweni La Wasichana Na Nyumba Ya Walimu Katika Shule Ya

Sekondari Maguvani,Kuzindua Daraja La Kijiji Cha Ilengititu,

Zahanati Ya Kichiwa Na vyoo  Vya Shule Ya Msingi Kichiwa Na Mradi

Wa Maji Katika Kijiji Cha Kifumbe.

Akizungumza Wakati Wa Kuweka Mawe Ya Msingi Katika  Miradi Wa

Surplise Beach  Na Maabara Ya Shule Ya Sekondari Sovi, Kiongozi Wa

Mbio Za Mwenge Kitaifa Kwa Mwaka 2015  Juma Khatibu Chum  Amesema

Serikali Inatambua Uwepo Wa Taasisi Za Watu Binafsi Pamoja Na

Jitihada Zinazofanywa Na Wananchi Katika Kutekeleza Miradi Kwa

Manufaa Yao Na Kutaka Jitihada Hizo Kuendelezwa.

Kwa Upande Wake Mkurugenzi Wa  Mradi Wa Kukuza Uchumi Na Utunzaji

Wa Mazingira Wa Beach Surplise  Patrick Alex Kyando  Amesema  Mradi

Huo Utakapo kamilika Unatarajia Kutoa Ajira Kwa Vijana Zaidi Ya 178

Ambapo Kwa Sasa Umegharimu Jumla  Ya Shilingi Milioni 605 Na

Unatarajia Kugharimu   Bilioni Mbili Na Milioni 17 Hadi Kukamilika

Kwake Mwezi Decemba 2018.







No comments:

Post a Comment