Sunday, June 7, 2015
Mkuu wa wilaya ya Mufindi amewataka wakazi wa mkoa wa Iringa kuwa walinzi namba moja dhidi ya wenyetabia ya kuharibu mazingira
Mkuu wa wilaya ya Mufindi Bi MBONI MHITA amewataka wakazi wa mkoa wa
Iringa kuhakikisha wanakuwa walinzi namba moja dhidi ya watu wenyetabia ya
kuharibu mazingira katika maeneo yao, kwani kwa kutofanya hivyo ni sawa na
kujiuwa wenyewe.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya habari na mawasiliano ya Halmashauri ya wilaya ya
Mufindi Imetanabasha kuwa, mkuu wa wilaya ameyasema hayo kwenye kilele cha
siku ya mazingira duniani yaliyofanyika kimkoa katika kijiji cha Vikula Wilayani
Mufindi Mkoani Iringa alipomwakilisha mkuu wa Mkoa kama mgeni rasmi.
MHITA amesema endapo wananchi hawata chukua hatua dhidi ya watu wenye
tabia ya za kuvuna miti kiholela, ufugaji wa mifugo usiozingatia taratibu za
kitaaluma, uchomaji moto ovyo, uharibifu wa vyanzo vya maji, uwindaji haramu
na ukataji mijti ovyo, kunauwezekano mkubwa wa kutoweka kwa misitu na
vyanzo vya maji nchini na kuhatarisha ustawi wa mwanadamu.
Aidha, ameyataja madhara yanayotokana na uharibifu wa mazingira kuwa ni
pamoja na mbadiliko ya hali ya hewa, kuongezeka kwa hewa ya ukaa, misitu
kuteketea kwa moto, kupungua kwa kiasi cha mvua na majra yake kubadilika
kuongezeka kwa joto sanjari na kupungua kwa mavuno mashambani.
Kaulimbiu ya siku ya mazingira mwaka huu inasema ndoto bilioni saba. Dunia moja . Tumia rasilimali kwa uangalifu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment