Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, June 15, 2015

DIWANI MJIMWEMA NJOMBE AKEMEA WIZI KWA WATOTO WADOGO ,ATAKA WAZAZI KUWA MAKINI

Diwani Wa Kata Ya Mjimwema Jimmy Ngumbuke Amewataka Wananchi Wa

Kata Ya Mjimwema Kuondoa Itikadi Za Kisiasa Katika Kusaidiana

Kwenye Matatizo  Mbalimbali Ambayo Yamekuwa Yakijitokeza Ikiwemo

Kusaidia Wagonjwa Wanapoumwa Ili Kudumisha Umoja Na Mshikamano

Katika Maisha Ya Kila Siku.

Akizungumza Na Uplands Fm Kuhusiana Na Tukio La Wizi Wa Mtoto

Katika Mtaa Wa Mjimwema Diwani Ngumbuke Amesema Kuwa Matatizo Hayo

Yanatokana Na Wananchi Wa Mtaa Huo Kuwa Na Itikadi Za Kisiasa 

Ambazo Zinasababisha Umoja Kutokuwepo Jambo Ambalo Amesema Wakati

Wa Kutekeleza Majukumu Ya Serikali Itikadi Zinatakiwa Kuondolewa Na

Kuwa Kitu Kimoja.

Aidha Bwana Ngumbuke Amesema Kuwa  Wananchi Wanapaswa Kuwalinda

Watoto Kama Watoto Wao Huku AKitaka Kufuata Maadili Yenye Kujenga

Na Kutaka Kuwasaidia Wagonjwa Katika Kuwachangia Michango Ili

Mgonjwa Apone Na Kuendelea Na Majukumu Ya Kitaifa Kama Ilivyokuwa

Hapo Zamani.

Bwana Ngumbuke Amesema Kuwa Kwa Sasa Wananchi Wengi Wamekuwa

Wakithamini Kuchangia Kwenye Misiba Na Siyo Ugonjwa Ambapo Ndugu

Wengi Wamekuwa Wakipoteza Maisha Kwa Kukosa Dawa Ya Shilingi Elfu

Kumi Na Nauri Ya Usafiri Hususani Wakazi Wa Vijijini Ambako Ni

Mbali Na Eneo La Huduma.

Bwa Ngumbuke Amesema Kuwa Juzi Kuna Dada Mwingine Alitaka Kutapeli 

Mtoto Katika Kituo Cha Afya Cha Njombe Mjini Baada Ya Dada Mmoja

Aliyekwenda Kupata Matibabu  Kuombwa Amuachie Mtoto Kwa Kuwa Mwenye

Mtoto Alikuwa Anataka Kuingia  Kwa Daktari Wakati Mtoto Akilia Na

Ndipo Aliposhitukiwa Kwamba Ni Mama Tapeli Ndipo Alipotokomea

Kusiko Julikana.

No comments:

Post a Comment