Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, February 4, 2015

UCHAGUZI WA MWENYEKITI WA CCM WILAYA PAMOJA NA MNEC WAFANYIKA WILAYANI NJOMBE

Chama Cha Mapinduzi Wilaya Ya Njombe  Kimefanikiwa Kufanya Uchaguzi Wa Viongozi Wake Wawili  Mwenyekiti Wa CCM Wilaya Na Mjumbe Wa Halmashauri Kuu Ya CCM Taifa NEC Kufuatia Kufariki Kwa Waliokuwa Wakishikilia Zafasi Hizo Ambao Ni Marehemu Adam Msigwa  Na Lupyana Fute.

Akitangaza Matokeo    Msimamizi  Mkuu  Na Mchumi Kwa Niaba Ya Kamati Ya Siasa Mkoa  Wa Njombe  Katika Uchaguzi Huo  Alimwimike  Sahwi  Amemtangaza Osca Michael  Msigwa Kuwa   Mjumbe  Halali Wa Halmashauri Kuu Ya CCM Taifa NEC  Baada Ya Kuongoza Kwa Kura Mia Saba 11 Kati Ya Kura 1171 Ya Kura Zote  Za Wapiga Kura.

Bwana Sahwi Amesema Nafasi Ya Mjumbe Wa Halmashauri Kuu Ya CCM Taifa NEC Waligombea  Watu  Watatu  Akiwemo Justin Nusulupia Ambaye Amepata Kura 337 ,Geoge Benedict Mng'ong'o  Amepata Kura 112  Na Oscar  Michael Msigwa Ambaye Ameongoza Kwa Kura  Mia Saba  11 Kati Ya Kura Elfu 1171 Dhidi Ya Wenzake.

Katika Hatua Nyingine Msimamizi Huyo Bwana Sahwi Amemtangaza Edward Pius Mgaya Kuwa Mwenyekiti Wa CCM Wilaya Ya Njombe Ambaye Ameongoza Kwa Kura  Elfu 1112  Kati Ya  Kura Zilizotakiwa Kupigwa  1174 Na Kura 29 Zimeharibika  Na  Kura Halali 1145   Dhidi Ya Mwenzake Bethren  Ngimbudzi Ambaye Amepata Kura 33.

Akizungumza Akiwa Mgeni Rasmi Mbunge Wa Viti Maalumu Mkoa Wa Njombe Na Naibu Waziri  Wa Maendeleo Ya Jamii,Wanawake ,Jinsia Na Watoto Dkt Pindi Hazara Chana Pamoja Na Kupongeza Kwa Zoezi Hilo  Pia Amesisitiza Wananchi Kujitokeza Kuipigia Kura Katiba Inayopendekezwa Ifikapo April 30 Mwaka Huu.

Naibu Katibu Mkuu Wa CCM  Tanzania Bara  Na Naibu Waziri Wa Fedha  Na  Mbunge Wa Jimbo La   Iramba Magharibi  Mwigulu  Lameck Nchemba Amesema Mkuu Wa Wilaya  Ya Njombe Anatakiwa Kuwa Makini Na  Oparesheni Zinazofanywa Na Halmashauri Za Kusafisha Miji   Wilayani Njombe  Kwani Wafanyabiashara Wadogo Wakiondolewa Katika Maeneo Yao Hawataweza Kupiga Kura Kuelekea Uchaguzi.


Baadhi Ya Wajumbe Wa Chama Cha CCM   Katika Maoni Yao Wameomba  Viongozi Waliochaguliwa Kushirikiana Na Wanachama Wote   Pasipo Kuwagawanya  Ambapo Uchaguzi Huo Wamesema Haukuwa Na  Kasoro  Kwani Wameridhishwa Na  Viongozi Waliochaguliwa.

Uchaguzi Huo Uliwashirikisha Wagombea  Watano  Walioingia Kwenye Kinyang'anyio Hicho Baada Ya  Wengine Kujitoa Na Kufariki Dunia Huku Wajumbe Wakitokea Maeneo Mbalimbali  Ya Kata Za Wilaya Ya Njombe  Umefanyika Januari 31 Katika Ukumbi Wa Hagafiro Mjini Njombe .

No comments:

Post a Comment