Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, February 9, 2015

MAJANGA JIMBONI KWA WAZIRI LUKUVI BWENI LA WASICHANA IDODI SEKONDARI LATEKETEA KWA MOTO


Wananchi na  wanafunzi  wa shule ya  sekondari  Idodi  Iringa   wakishiriki  kuzima  moto katika  bweni la  wanafunzi  wa  kike  shuleni  hapo amnbalo lilikuwa  likiwaka  moto  leo  asubuhi
MOTO  mkubwa  ambao  chanzo chake  kinatajwa  kuwa  ni  hitirafu  ya  umeme  umeteketeza bweni  la  wasichana  katika  shule  ya  Sekondari  Idodi  wilaya  ya  Iringa  mkoani Iringa .

Tukio hilo  limetokea  muda  wa saa 4  asubuhi  leo wakati  wanafunzi  wakiwa  wakiwa madarasani  wakiendelea na masomo.

Akizungumza na mtandao  huu  wa www.matukiodaima.co.tz ,kamanda wa jeshi la Zimamoto Mkoani Iringa, Inspekta Kennedy Komba alisema kuwa bweni hilo limeteketea lote na kuunguza mali zilizoko katika bweni hilo na chache kuokolewa na wananchi waliowahi kufika eneo la tukio kusaidia  kuzima moto  huo.

Alisema kuwa chanzo cha moto huo imesababishwa na hitalafu ya umeme na hakuna mwanafunzi yoyote aliyejeruhiwa na moto huo.

Komba alisema kuwa baada ya jeshi la zimamoto kupata taarifa waliondoka mjini Iringa ambapo  ni  zaidi ya  kilometa 20 hadi  ilipo shule  hiyo  ili  kwenda  kuzima  moto  huo.

Hata  hivyo  aliwapongeza wananchi kwa moyo wa ushujaa kujitolea kuzima moto huo na kuwataka kutoa taarifa mapema pindi majanga ya moto yanapojitokeza katika maeneo yanayowazungu.

“Endapo tungepata taarifa mapema nina amini tungeweza kuokoa vitu vingi zaidi na kuwataka wananchi wasitegemee mtendaji au kiongozi apige simu katika kikosi cha kuzima moto kwani kila mtu ana haki ya kupiga simu 111 katika kitengo cha mawasiliano cha jeshi hilo kuweza kutoa taarifa ya majanga, tumetumia muda mdogo kufika eneo la tukio kutokana  ubora wa gari hivyo nawashukuru sana wananchi kwa taarifa na kuweza kuonyesha ushirikiano katika uzimaji wa moto huo usilete madhara zaidi “ alisema

Akizungumzia hasara iliyosababishwa ni kiasi gani Komba alisema hadi sasa hawajapata tathmini kamili ya mali zilizoteketea ila baada ya kazi kukamilika itafahamika ni thamani ya vitu vilivyoungua na kuwekwa wazi kwa wanachi.

Mbunge  wa   jimbo la Isimani Wiliam Lukuvi ambako maafa  hayo yametokea  mbali ya  kuwapa  pore  walimu na  wananchi  wa  Idodi  kwa tukio  hilo  bado  aliwapongeza  wananchi  kwa  umoja  wao kwa  kufika mapema  kuthibiti  moto  huo pamoja na kikosi  cha  Zimamoto kutoka mjini Iringa.
Tukio  hilo kubwa  kulikumba  jimbo la Isimani  linaloongozwa na  mbunge  wake  Wiliam Lukuvi ambae ni  waziri  wa  nyumba na ardhi 
 
Akizungumza  kwa niaba ya mbunge  Lukuvi katibu  wa  mbunge  huyo  Thom Malenga  alisema  kuwa  wananchi  wamefanyajitihada  kubwa katika  kuthibiti  moto  huo na  kuwa mbali ya mali za  wanafunzi  hakuna madhara  kwa  binadamu.

Kuhusu  thamani ya mali  zilizoteketea  kwa  moto  huo  alisema  kwa  sasa  bado mapema  kujua  ila uongozi  wa  shule  hiyo pamoja  na  wazazi na  wananchi wa Idodi  wapo katika  kikao ili  kujua madhara  zaidi  na hasara  iliyojitokeza.

Japo  alisema  hasara za  awali  zinaonyesha  ni  vitanda  vyote  zaidi ya  90  pamoja na baadhii ya vifaa  vya  wanafunzi  vimeteketea kwa  moto  huo na  kuwa  jumla ya  wanafunzi  zaidi ya 110 hawana mahali  pa  kulala.

Alisema  kuwa mwaka 2009  baada ya  bweni la  wasichana  kuteketea kwa  moto  uongozi  wa  shule  hiyo  uliamua kuwabadilishia  wanafunzi  wa  kike bweni na  hivyo  bweni  hili  lilikarabatiwa na  kupewa  wavulana.

 Agosti 25/ 2009  jumla  ya  wanafunzi 13  walipoteza maisha baada ya  bweni lao  kuteketea kwa  moto na  baadhi  yao  kujeruhiwa kwa ajali  kama  hiyo ya  moto ambayo kwa  kipindi hicho moto  huo ulisababishwa na mshumaa.
Chanzo  Francis Godwin Blog -Iringa


No comments:

Post a Comment